Rais Barack Obama kamponda Muwania Urais wa Republican Donald Trump, ataka Mienendo yake Ichunguzwe


Rais Barack Obama ataka mienendo ya muwania Urais wa Republican Donald Trump ichunguzwe, asema urais sio maigizo.

Obama amesema matamshi ya mwanasiasa huyo yanafaa kuchukuliwa kwa uzito na kuwekwa kwenye mizani ili Wamarekani wapime iwapo anafaa kuwa Rais au hafai.

Obama amesema kauli za Trump haswa katika maswala ya usalama wa taifa na sera za kigeni ni za kutiliwa shaka na kusisitiza kuwa: "Urais hapa nchini sio mchezo wa kuigiza." Kadhalika Rais wa Marekani amevitaka vyombo vya habari kutoangazia tu kile alichokitaja kuwa kauli za kisanii za mwanasiasa huyo bali viangazie pia matamshi yake ambayo yanaweza kuzusha vita, kutia doa uhusiano wa Washington na nchi zingine na kuvuruga mfumo wa uchumi wa Marekani.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: