Uongozi Wa Juu Wa CCM Watoa Kauli kuhusu viongozi waliotajwa sakata la mchanga wa madini


Chama Cha Mapinduzi (CM) kimewataka viongozi na wote waliotajwa katika sakata la mchanga wa madini kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola baada ya kutuhumiwa kulisababishia Taifa hasara kubwa ya matrilioni ya fedha kutokana na usafirishaji wa mchanga wa madini kwenda nje ya nchi.

Hayo yalielezwa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za chama hicho Lumumba jijini Dar es Salaam.

Aidha, Polepole alisema kuwa, chama hicho hakitasita kuwachukulia hatua kwa wanachama wake iwapo watabainika kuliingizia taifa hasara kupitia njia mbalimbali ikiwamo hii ya sasa ya kupitia mchanga wa madini. 
Polepole amesema kwa sasa chama kinaviachia kwanza vyombo vya dola vifanye kazi yake ya kuwahoji waliotajwa kwenye ripoti hizo mbili.

CCM imepongeza Rais Dkt John Pombe Magufuli ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho kwa jitihada kubwa anazofanya katika kuhakik

“Rais Magufuli anafanya kazi ya kuweka mifumo ya kusimamaia na kudhibiti shughuli za migodi ili zifanye kazi kwa mujibu wa sheria na kusimamia masilahi ya watanzania na kuhakikisha tunakomesha utoroshhwaji wa madini. Anatekeleza ilani ya CCM kifungu cha 35 kinachotaja kukomesha utoroshwaji madini katika nchi yetu,” alisema na kuongeza.

“Niwahakikishie CCM sio serikali ya kinyonge hasa tunaposimamia masilahi mapana ya watanzania. Huyu John kapanda ndege amekuja kusikiliza shutuma za kampuni yake tanzu na tumeridhidhwa na uamuzi huu wa kampuni yake kukiri makossa.”

Aidha, Polepole alisema CCM haitasita kuchukua hatua kwa watakaothibitishwa na vyombo vya dola kwamba wameshiriki katika sakata hilo, kwani chama hicho kinaongozwa na kanuni ya uongozi na maadili na kwamba kitendo hicho ni kinyume na maadili ya katiba ya chama hicho.

“CCM inaongozwa na katiba, kanuni na sheria. Kanuni yetu ya uongozi na maadili inalenga kuweka msingi wa ujenzi wa jamii ya viongozi wanaosimamia haki, wanaochukia rushwa na kupiga vita ubadhirifu wa mali ya umma, hivyo kitendo hicho ni kinyume na katiba yetu. CCM  ni wadau wa kwanza kusubiri matokeo ya vyombo vyetu mbalimbali vya kiuchunguzi, ikionekana kuna shida tunazo taratibu na chama hakitasita kuchukua hatua,” alisema.

Aliongeza kuwa “CCM inatoa rai, kwa baadhi yetu ambao wanataka kuugeuza mjadala huu muhimu kwa taifa letu kuwa siasa, kwa kutoa hukumu kwa viongozi wetu, wakuu wa nchi wa serikali na maamiri jeshi wetu wakuu wastaafu ambao wamefanya kazi kubwa ya ujenzi wa taifa hili,tuwaache hawa viongozi wapumzike, tusonge mbele kusimamia haki ya watanzania.”
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: