picha mbali mbali Diamond ,Mafikizolo na mawazil, baada ya kutoka bungeni,Diamond Platnumz kaipongeza sana serikali,









Diamond Platnumz amedai kitendo cha serikali kuwapa nafasi kuja bungeni leo kumeonyesha jinsi gani serikali inajali vipaji vya Tanzania hivyo hiyo ni picha nzuri ambayo wasanii hao wa kundi la Mafikizolo wataondoka nayo pindi watakapo rejea nyumbani kwao.
"Unajua leo tuna show hapa Dodoma mimi na Mafikizolo hivyo serikali kupitia kwa Waziri Nape Nnauye walitualika bungeni japo ni kwa muda mchache lakini kitendo hiki kinaonyesha jinsi gani serikali yetu inajali wasanii, unajua hawa wenzetu wanapokuwa kwao na sisi tunapokwenda huwa tunapata mapokezi mazuri sana hivyo na mimi nashukuru kwa hili kwani itafanya hata wenzetu wajue serikali yetu inajali wasanii wake". alisema Diamond Platnumz.




"Kesho na kesho kutwa wenzetu wakirudi kwao watasema wale wenzetu wale serikali yao inawajali na kuwa support wasanii wake kwani tulikwenda tukapata nafasi kwenda mpaka bungeni na watasimulia mambo mbalimbali ambayo wao wamejionea hivyo ni kitu kizuri" aliongezea Diamond Platnumz
 


Mbali na hilo Diamond Platnumz alielezea wimbo wao huo wa pamoja ambao unaitwa 'Colours of Africa' ni wimbo ambao unazungumzia tamaduni za Kiafrika, ushikamano na umoja wa bara la Afrika.
 
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: